Harmonize Ajivunia Kwangaruu Nchini Kenya.
Msanii wa muziki kutoka katika kundi la WCB anajivunia kufanya vizuri kwa wimbo wake wa kwangaru ambao alimshirikisha bosi wake Diamond Platinumz.
Harmonize ambae yuko nchini humo kwa ajili ya kufanya tour ya wimbo huo anasema katika kila sehemu anayofanya show anaona kuwa na mwitikio mkubwa na mashabiki wamekuwa wakijitokeza kwa wingi.
Harmonize anafurahi zaidi anapoona kuwa kila anapopanda jukwaani kuimba wimbo huo , mashabiki wamekuwa wakiuimba mwanzo mwisho, kitu kinachompa matumaini zaidi.Na hata baadhi ya watu wamekuwa wakisema kuwa wimbo huo ndio wimbo wa mwaka.