Harmonize Amkingia Kifua Mobetto Baada Ya Kugeukwa na Kila Mtu

Staa wa muziki wa Bongo fleva Harmonize ameonekana kuwa upande wa Hamisa Mobetto na kumkingia kifua baada ya kila mtu kumtolea povu.

Sakata hili lilianza siku ya Ijumaa baada ya  Diamond kuachia wimbo na video yake mpya ya wimbo unaoitwa Iyena aliomshirikisha Rayvanny ambapo ndani ya wimbo huo Video Queen ni Zari.

download latest music    
Baada ya video hiyo kutoka karibia kila mtu kuanzia familia ya Diamond mpaka WCB wote walianza kumposti Zari huku wakimtaka arudi kwa Diamond na kumponda kabisa Hamisa.
Harmonize pekee alionekana kuwa upande wa Hamisa kwani baada ya kila mtu kwenda upande wa Zari Harmonize alimpa moyo Hamisa ambapo aliandika ujumbe huu:

Lakini pia hata Kwenye mahojiano aliyofanya na WAsafi Tv Harmonize alipoulizwa kwanini peke yake ameamua kuwa uapnde wa Hamisa alijibu kuwa yeye ni kama bendera fuata upepo kwani Diamond alisema yupo na Hamisa basi atakuwa upande huo na alisema kwa MObetto na yeye atakuwepo huko.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.