Harmonize apiga show nyumbani kwao Mtwara, hivi ndivyo mashabiki walijitokeza (Picha)

Iwapo kuna msanii ambaye anatambulika Afrika Mashariki ni Harmonize. Hii ni kwa sababu ni mmoja wa wasanii kutoka WCB na pia kwa sababu ya mchumba wake anayetambulika kwenye muvi za bongo, Wolper.

Hata hivyo weekend hii Harmonize alijiunga na wasanii wengine kupiga show nyumbani kwao Mtwara. Mbali na show hii yake msanii huyu alikuwa amepanga kutembelea Hospitali ya Mkoa kuwaona wagonjwa na pia kuwasaidia baadhi ya wale ambao walikuwa wanahitaji fedha.

download latest music    

Kulingana na picha zilizochukuliwa katika show hiyo, inaonekana kuwa Harmonize alikuwa amewavutia wengi na ingawa Young Killer, Shilole na Aunty Ezekeli walikuwepo… mashabiki hawa walimtambua Harmonize zaidi.

Tazama picha hizo hapa.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua