Harmonize Asema Hana Bifu na Mwarabu Fighter
Kulikuwa natuhuma za kuwa mwanamuziki harmonize hana mahusiano mazuri na body guard wao kwa sababu ya tetesi zilizowahi kusambaa kuwa alikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na sarah ambae ni mpenzi wa harmonize.
Akiongea na waandishi wa habari siku ya jana , Harmonize alifunguka na kusema kuwa Yeye na mwarabu fighter hawana mahusiano mabaya wala ugomvi wowote na hata maneno mabaya aliyowahi kuzushiwa yalikuwa hayana ukweli wowote.
katika mahojiano yaliyowahi kupita huku nyuma, sarah, mwarabu fighter na hata harmonize mwenyewe aliwahi kukanusha taarifa hzio na kusema kuwa maneno hayo hayana ukweli wowote.