Harmonize Atangaza Ujio Wa Albamu Yake

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB, Harmonize ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake wa ‘Kwangaru’ ametangaza ujio wa albamu.

Harmonize ametangaza Habari hiyo njema kwa mashabiki zake wanaopenda muziki wake kwani hiyo ndio itakuwa albamu yake ya kwanza tangu aanze kufanya Muziki.

download latest music    

Kwenye Interview yake na Bongo5, Harmonize amefunguka kuwa analazimika kutoa albamu kwa sababu ndio utambulisho rasmi wa msaniii ndani ya tasnia ya muziki.

Nipo ndio nashughulikia albamu yangu lakini nipo kwenye hatua za mwisho sana, so muda wowote naweza kuitangaza lini itatoka, itakuwa na wasanii tofauti tofauti“.

Siku za nyuma Diamond Platnumz alishawahi kufunguka kuwa wasanii wote wa WCB wanatoa Albamu zao kwa muda fulani ambapo yeye ameshatoa albamu yake ya ‘A boy from Tandale’.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.