Harmonize- Nipo Tayari Kumuoa Sarah

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize amefunguka na kuweka wazi mipango yake ya kumuoa mpenzi wake Sarah.

Kwa muda mrefu kumekuwa na maneno mengi kuhusu Mahusiano ya Harmonize na Sarah huku wengi wakidai Harmonize hana mapenzi ya kweli kwa Sarah bali yuko naye kwa ajili ya pesa.

download latest music    

Huku dhana hiyo ikiwa imepandikizwa na Ex wa Harmonize, Jacqueline Wolper ambaye alisema Harmonize alianzisha Mahusiano na Sarah wakati wako pamoja kwa sababu alikuwa anamuwezesha kifedha.

Lakini Harmonize ameibuka na kuweka wazi kuwa anampenda Sarah na hivi sasa yuko tayari kumuoa mwanamke wake huku akipuuzia maneno yote ambayo yanasemwa na watu.

Kwenye mahojiano na The Playlist ya Times Fm, Harmonize aliweka wazi mipango yake ya ndoa baada ya kuulizwa na Lil Ommy kama ana mpango wa kumuoa Sarah:

Ndiyo nataka nimuoe Inshallah”.

Harmonize anafanya vizuri na nyimbo zake mbili ambazo ni Kwa ngwaru aliyomshirikisha Diamond Platnumz na wimbo wake mpya Dm Chick ambao amemshirikisha Sarkodie.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.