Harmorapa Apata Dili Nono la kuwa balozi
Msanii wa bongo fleva Harmorapa amepata dili kubwa katikamoja ya kampuni za usafirishaji nchini inayojulikana kama moovin.
Kampuni hiyoimemtangaza Harmorapa na moja ya watangazaji wa kipindi pendwa katika Clouds Media cha XXL kama mabalozi wao kwa sasa katika maswala na huduma wanazotoa katika jamii.
Akiongea baada ya kutangazwa kuwa balozi wa kampuni hiyo, Harmorapa anasema kuwa anamshukuru mungu na kampuni hiyo kwa kutambua nafasi yake katika kufanikisha huduma zao na anaamini kuwa nafasi hiyo itamfungulia milango mingine mingi.
Hamorapa aliwahi kuwa balozi wa kinywaji cha swala hapo awali ambapo mkataba wao uliisha.