Harmorapa: Naamini Kuna Siku Wema Sepetu Atakuwa Mpenzi Wangu

Mwanamuziki na rapa anayeongoza kwa kupenda kiki ‘Harmorapa’ amerudi tena kwenye vichwa vya habari na kufunguka kuwa ana imani kuwa ipo siku atakuja kumuoa muigizaji wa Bongo Movie, Wema Sepetu.

Siku za nyuma kidogo Harmorapa hakusita kuweka hisia zake hadharani na kusema kuwa anampenda Wema Sepetu na ndoto yake kubwa maishani ni kumuoa na awe mke wake, kitu ambacho kilimpa sana harmorapa lakini Wema aliibuka na kumkataza Harmotapa kutumia jina lake ndipo pale Harmonize alipogeuza kibao na kuanza kumponda Wema kwa kumuita Bibi.

download latest music    

Siku mbili zilizopita Harmorapa aliibuka tena na kuonyesha hisia zake kuwa hata kama muda umepita Lakini bado hisia zake juu ya Wema ziko pale pale. Harmorapa amedai kuwa naye anaamini ipo Siku atatimiza ndoto yake ya kumuoa Wema kama Dogo Janja alivyobahatika kumuoa Uwoya.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Harmorapa alifunguka mazito juu ya kipenzi chake Wema:

Dah Naamini sana katika ndoto, kuwa ipo siku ndoto unayoota kuwa kuja kweli sina la kuongeza zaidu ya kumpa hongera Dogo Janja kwa kutimiza ndoto yake ya kumuoa Irene Uwoya naamini ushupavu wake na kumemfanya kutokuvunjika moyo ndio kumemfanya leo hii akawa mume wa mwanamke wa ndoto zake…Nami sivunji imani naamini ipo Siku Wema Sepetu atakuwa wangu ugumu alioupata Janjaro umenipa matumaini kikubwa ni kutulia na ndoto yangu  na kulenga ipo siku itatimia…one day you will be mine Wema Sepetu”.

Baada ya Dogo Janja kufanikiwa kumuoa Uwoya ameonekana nimfano wa kuigwa kwa vijana mbali mbali huku akiwapa somo la uvumilivu na kuamini kuwa ipo Siku yatatimia, Wema Sepetu hajamjibu bado Harmorapa lakini inajulikana kabisa Wema atakuwa hajafurahishwa na kitendo hicho.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.