“Haters Wanazidi Kunipa Umaarufu na Kuniongezea Dili za Pesa” -Hamisa

Mwanamitindo na Muigizaji wa Bongo movie Hamisa Mobetto amewatolea povu zito wale wote wanaomsema vibaya na  kumponda kwenye mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Mwananchi Communication Limited Hamisa amefunguka na kusema anawashangaa zaidi haters ambao wamekuwa na kazi ya kumchafua kila siku hasa wale wanampachika majina mapya kila siku.

download latest music    

Hamisa amedai hivi sasa ameshayazoea majina yote anayopewa na mashabiki Kwenye Instagram kwani ameona hayampunguzii kitu katika maisha yake labda cha zaidi yanamuongezea umaarufu unaozidi kumpa deals mbali mbali za kuingiza pesa.

Kutokana na bifu mbali mbali za mtandaoni na mashabiki kugawanyika kimakundi huunda timu zao binafsi kama Teamwema, Teamzari na teamMobetto. Ambapo Hamisa amepewa majina mbalimbali kama Tununu, laki mbili, ruba hata mbu.

Baada ya kuzaa na Diamond Hamisa alipata haters wengi ambao walimtunga majina mbali mbali na kumsema vibaya ambapo amesema vimemsaidia kumpa mafanikio kwani hivi sasa ana mafanikio mengi ikiwemo kuwa balozi wa website ya Mzuri ya Kenya na hata kufanya Safari nchi mbali mbali kama Dubai, South Africa, na hata Uganda kwa kazi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.