Hatimaye Diamond Amuweka Mtoto Wake na Hamisa Mtandaoni

Mwanamuziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz anayefanya vizuri na kibao chake cha kwangwaru ametengeneza gumzo Kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuposti picha ya mtoto wake na Hamisa.

Hatimaye kwa mara ya kwanza Diamond ameposti picha ya kwanza ya mtoto wake Dylan ambaye amezaa na Hamisa.

download latest music    

Tangu Dylan azaliwe kulikuwa na mgogoro kati ya Diamond na Hamisa hii ilitokana na Hamisa kuanika video na picha zao za faragha Wakati huo Diamond alikuwepo na Ex wake Zari.

Tangu hapo kilichofuata kilikuwa ni kurushiana vijembe Mtandaoni na kupelekana mahakamani na hata Hamisa alisema kuwa Diamond alikuwa hataki kumuona mwanaye na hata kumuhudumia.

Lakini tangu taarifa za Diamond na Hamisa kurudiana zienee inaelekea mambo yamekuwa tofauti kwani Diamond amesemekana hata kumuona mtoto wake na hata jana kwa mara ya kwanza aliweza kumposti mtoto wake Kwenye ukurasa wake wa Snapchat:

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.