Hatimaye Mama Diamond Amkubali Mtoto wa Hamisa Kuwa Mjukuu Wake

Mama mzazi wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi Sandra au maarufu kama Mama Diamond amemkubali mjukuu wake Dylan kwa mara ya kwanza hadharani.

Dylan ni mtoto wa mwisho wa Diamond aliyezaa na Hamisa kipindi bado yupo Kwenye Mahusiano ya kimapenzi na mama watoto wake aliyezaa naye watoto wawili Zarinah Hassan.

download latest music    

Kwa muda mrefu imekuwa ikonekana kama Mama Diamond hana mapenzi kwa mjuukuu wake Dylan kutokana na kuwaposti watoto wa Zari Tiffah na Nillan tu Kwenye mitandao ya kijamii.

Mama Diamond aliwahi kuweka wazi kuwa anamchukia Mama Yake na Dylan Hamisa Mobetto na hata kusemekana kumtembezea kipigo kizito na sababu ni Hamisa kumuita Mama Diamond Shilawadu.

Wikiend iliyopita ilikuwa Birthday ya Mama Diamond ambapo Diamond alimuandikia Mama yake ujumbe mzito akimtaka amsamehe Hamisa na amkubali mjukui wake Dylan na ampende kama wajukuu zake wengine.

Maneno hayo ya Diamond yameonekana kumuingia mama yake kwani Kwenye clip ya birthday yake ameonekana akipokea Keki kutoka kwa Dylan na akimuita Dylan mume wake na Kukiri kuwa anampenda.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.