Hatimaye Ray C akutana na Rayvanny na Diamond Platnumz

Image: Ray C

Mwimbaji mkongwe, Ray C, aliweza kukutane na wmibaji anayempenda sana Rayvanny hivi majuzi wakiwa HQ ya Wcb_wasafi baada kikao juu ya sanaa.

Kupitia mtandao wa Instagram, Ray C aliweka video yake na Rayvanny wakiimba na kulingana na tabasamu yake mwibaji huyu alikuwa ameeingojea siku hii kwa hamu na ngamu.

download latest music    

Kwa muda sasa Ray C amekuwa akitamani kufanya kazi na kijana huyu wa Wasafi records na hivi sasa kuna dalili kuwa wawili hao wanauwezo wa kuachilia nyimbo pamoja.

Ingawa Ray C alikuwa na shida na management yake, hivi sasa nyimbo zake zinawaweza kupatikana katika mtandao mpya wa wasafidotcom.

Mama Saida Karoli na Professor Jay pia walikuwa katika kikao hiki kilicho fanyika Jumanne iliyopita. Tazama video ya Ray C na Rayvanny hapa.

??????????

A post shared by Ray C (@rayctanzania) on Mar 14, 2017 at 1:06pm PDT

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua