Hatimaye Wastara Afanikiwa Kwenda Nje Kwa Matibabu.

Msanii wa bongo movies ambae pia kwa sasa amejiingiza katika sanaa ya nyimbo Wastara Juma amefanikiwa kupata ela yote aliyokuwa anatakiwa kuikusanya kwa ajili ya matibabu yake yanayotakiwa kuanza punde atakapofika nje ya nchi.Wastara ambae amekuwa akilia kila siku katika vyombo vya habari ili awezi kupata fedha kwa ajili ya matibabu amesindikizwa jana uwanja wa ndege kwa ajili ya kwenda nchini India.

Akiongea na waandishi wa habari Wastara amewashukuru sana wananchi waliojitokeza kwa ajili ya kufanikisha ukusanyaji wa fedha hizo ikiwa ni pamoja na Mh.Raisi ambae alitoa zaidi ya milioni 10 kwa ajili ya kuchangia pale panapohitajika.

download latest music    

Nawashukuru sana wananchi na pia vyombo vya habari, kwa muda mrefu sana nimekuwa nikiongea na kuonekana kwenye vyombo vya habari na ninaamini kuwa bila wao mimi nisingekuwa wastara.bila wao nisingekuwa hapa uwanja wa ndege ninaenda kutibiwa , ninawashukuru sana kwa moyo mkubwa walonionyesha.-Aliongea Wastara huku akilia kwa uchungu.

Wastara amekuwa akilia kwa uda mrefu kutokana na maumivu ya mgongo anayokuwa anayapata kwa muda mrefu sana kutokana na ajali aliyoipta miakamingi na kusababishwa kukatwa mguu wake mmoja na kuwekewa vifaa kwa ajili ya kumsapoti kutembea.

Wastara aliamua kufunguka katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuhgusushida yake hiyo kuwa peke yake hatoweza kufanikiwa kupata ela zinazohitajika kwa matibabu hivyo aliwaomba wananchi wamsaidia kumchangia na kupata ela hizo,ombi amablo lilipokelewa vizuri na wananchi na viongozi mbalimbali na kumsaidia kupata fedha hizo.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.