Hawa Afunguka Baada Ya Diamond Kumpa Milioni 50 Za Matibabu

Msanii wa Bongo fleva Hawa Mayoka aliyewahi kutamba katika ngoma ya Diamond Platnumz ‘Ntarejea’ amefunguka na kumshukuru Msanii huyo kwa msaada wake wa matibabu.

Wiki chache zilizopita Habari zilisambaa kuwa Hawa anaumwa hoi kitandani na kuomba msaada wa matibabu ambapo tatizo ni  ini.

download latest music    

Diamond amethibitisha Kupitia mitandao ya kijamii kuwa yupo katika harakati za kumpeleka Hawa nchini India kwa ajili ya matibabu na kusema anatoa zaidi ya Milioni 50 kwa ajili ya matibabu yake kutoka katika mfuko wake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda,  Hawa amesema kitendo cha Diamond kujitolea kumsaidia matibabu ya kumpeleka nchini India kimemliza mno kwa sababu hakujua kama ipo siku angemkumbuka.

Nilivyosikia Diamond ameamua kunisaidia nilijisikia furaha mpaka machozi yakawa yananitoka maana sikuamini, Mungu atamlipa na namuombea azidi kuwa na moyo huohuo.

Nilishakata tamaa kabisa ya kupata matibabu kutokana na uwezo wa kifedha kuwa mdogo kwani madaktari wa hapa walisema natakiwa kutibiwa India, kwa sasa nimepata tumaini jipya baada ya Diamond kujitolea kunipeleka kwenye matibabu India“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.