Hawa Asimulia Alivyonusurika Kifo

Afya ya Hawa kwa sasa imeimarika na kurudi katika hali yake ya kawaida baada ya kuchungulia kaburi, jambo ambalo hata yeye mwenyewe hakulitegemea kwani alishakata tamaa ya kuishi. Mwishoni mwa mwaka jana, Hawa alipelekwa kwenye matibabu nchini India kutokana na tatizo lake la tumbo kujaa maji.

Jitihada hizo za matibabu ya Hawa zilifanywa na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ aliyeshirikiana naye kwenye Wimbo wa Nitarejea. Baada ya kurejea Bongo, Hawa aliwekwa mafichoni kwenye hoteli moja jijini Dar kutokana na maelekezo kutoka kwa madaktari ambao walitaka iwe hivyo kwa miezi mitatu.

download latest music    

Baada ya miezi hiyo mitatu, Hawa alirejea nyumbani kwao, Buguruni-Rozana jijini Dar kuendelea na maisha yake kama kawaida. Risasi Mchanganyiko lilimuibukia nyumbani hapo ili kufanya naye mahojiano kuhusu hali yake kwa sasa na mambo aliyoyapitia.

“Kwa kweli ninamshukuru sana Mungu maana bila yeye, huenda nisingekuwepo, leo hii naweka tabasamu usoni, lakini niliteseka mimi jamani. Hadi ninasafiri kwenda India nilikuwa na maumivu makali hadi nilihisi kama nataka kuchanganyikiwa, yaani hadi kumsimulia mtu nahisi kama nitampunja kwa sababu hayaelezeki, yalikuwa makali sana. 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.