Hii ndio sababu Linex hajaweza kuachia nyimbo mpya

Linex ambaye ni msanii wa Bongo ameweza kuachia nyimbo kadhaa ambazo zimetamba Afrika Mashariki kwa muda sasa. Lakini inaonekana kuwa ameweza kuwa kimya kwa miezi kadhaa bila kuachia nyimbo yoyote hata hivyo msanii huyu amefunguka kuelezea sababu zake za kutoweka mambo mpya.

Akizungumza kwenye kipindi cha Twenzetu Linex alisema kuwa alijipa muda wa kupumzika kwa sababu tangu aanze kuimba miaka 7 iliyopita hajapata saa ya kukaa nyumbani na kutulia na familia yake. Alisema,

download latest music    

“Kwa hiyo ninaweza kurudi muda wowote, sisemi kuwa nitakaa muda mrefu bila kutoa wimbo kwa sababu kuna vitu nilitakiwa kuvifanya lakini sikuvifanya ambavyo ni mapumziko, nimefanya kazi zaidi ya miaka saba sijawahi kukaa nyumbani hata siku mmoja,”

Aliendelea kwa kuongeza,

“Kwa hiyo nimejipa mapumziko huu ni mwezi karibia wannne sasa, nimekaa nyumbani nimepumzika, nimeandika kazi, kwa hiyo any time nitafanya kitu ambacho ni kikubwa.”

 

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua