Huddah Afungukia Mahusiano Yake na WCB

Socialite maarufu kutoka Kenya mrembo Huddah Monroe maarufu kama Huddah The Bosschick amefungukia uhusiano wake na Label maarufu nchini WCB.

Huddah alitua nchini Tanzania mwishoni mwa wiki hii na mara moja alionekana akiwa katika ofisi za WCB na CEO wake staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi The Playlist ya Times FM, Huddah amesema kuwa ukiachilia mbali sababu za kibiashara, amekuwa akivutiwa na uchapakazi wa timu nzima ya WCB.

The vibe is, WCB napenda sana ni watu wanajima, watu wana njaa ya maisha , so for me WCB have the some kind of vibe the i have. Wanapenda maisha mazuri, so they very work hard hawalalai saa 24 wapo kwenye kazi, so that I like that”.

Huddah ambaye ni Mfanyabiashara anayemiliki make up line yake inayoitwa Huddah Cosmetics ambayo imekuwa ikifanya vizuri.

Huddah Monroe alikuja nchini Tanzania kwa ajiili ya ku-host show ya Harmonize iliyofanyika siku ya leo June 16, 2018.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.