Huu ndio ujumbe Diamond Platnumz amemwandikia professor Jay kupitia Instagram

Image: Diamond Platnumz

Diamond Platnumz amewaacha wengi wakishangaa baada ya ujumbe aliomwandikia mbunge wa Mikumi Joseph Haule a.k.a Prof Jay. Msanii huyo wa Wasafi records aliandika kumwambia Prof Jay sababu ambazo yeye hakujitolea kutumbuiza kwenye kampeni zake mwaka uliopita.

Hit maker wa Marry me aliandika kusema,

download latest music    

“Ndio Maana kwenye Jimbo lako sikuja kupiga kampeni bro…kwakuwa niliijua mapema thamani na umuhimu wa Uwepo wako kwenye hilo jengo….. @professorjaytz

Hata hivyo wengi wasichokielewa ni kwa nini msanii huyo alimchana mwenzake ata baada ya yeye kumshughulikia bungeni baada ya kudaiwa kuwa anadeni la TRA la milioni 400.

Wasanii wengine hata hivyo wamekuwa wakimuunga mkono Prof Jay ambaye anawashungulikia wasanii kwani pia yeye anaelewa shida ambazo wao hupitia.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua