Idris Sultan Amwagia Misifa Kibao Shilole

Mchekeshaji na msanii wa Bongo movie Idris Sultan ameibuka na kumwagia sifa kibao Msanii wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole.

Siku ya jana ilikuwa ni siku ambayo Shilole alikuwa a ashehereka siku yake ya kuzaliwa na mastaa mbali mbali walimposti katika kurasa zao kwenye mitandao ya kijamii.

download latest music    

Mmoja wapo ni Idris Sultan ambaye alimposti na kumuandikia ujumbe mzito ambapo ndani ya ujumbe huo alindika ni Jinsi gani msanii huyo ni mchapakazi na anajituma tofauti na mastaa wengine.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Idris Sultan aliweka picha ya Shilole na kuandika ujumbe huu kumlenga Shilole:

Ana Nyumba, ana biashara zaidi ya tatu, ana watoto, ameolewa na ni maarufu na bado ana baby face, Mimi Nina kingereza tu. Tuendelee kuendekeza ujinga tutajua nani anamcheka mwenzake”.

Mbali tu kuwa msanii wa Bongo fleva na Bongo movie, Shilole pia ni mjasiriamali ambaye ni ana mgahawa wake anapouzia chakula pia anamiliki bidhaa zake mwenyewe kama vile Chili na nyinginezo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.