Irene Paul Ana Matatizo Yake Binafsi- Rammy Galis

Muigizaji wa Bongo movie Rammy Galis ameibuka na kujitetea baada ya sakata lake la kutuhumiwa kuigiza amezimia na msanii mwenzake Irene Paul kwenye msiba wa Agnes Masogange.

Siku ya Jumapili pale Leaders Club ambako Marehemu Agnes Masogange alikuwa anaagwa kuliibuka kizaazaa baada ya Rammy kupoteza fahamu hali iliyopelekea abebwe na kupelekwa kwenye gari kwa ajili ya huduma ya kwanza.

download latest music    

Lakini baada ya sakata hilo msanii wa Bongo movie Irene Paul alishangaza watu wengi baada ya kuamua kumshambulia Rammy na kumtuhumu kwa kujifanyisha na kupeleka maigizo msibani na kudai alikuwa hajazimia bali alikuwa anatafuta kiki.

Kwenye mahojiano na Dizzim Online, Rammy amejitetea kuwa kitu kilichomfanya azimie ilikuwa ni kuchoka baada ya kusimama kwa muda mrefu hivyo kuishiwa nguvu kabisa lakini pia ameweka wazi kuwa Irene Paul ana matatizo naye tangu siku nyingi:

Mimi sina matatizo na Irene kwa sababu kwanza Mungu alinijalia mini kuwa mwanaume na yeye kuwa mwanamke kwaiyo siwezi kubishana na mwanamke lakini huyu ana matatizo yake binafsi kwa sababu hata tukiwa location tumegombana sana na ninaweza kusema alikuwa ana matatizo na marehemu pia kwa sababu aliwahi kuniambia unaishi na mtu unajua nani anamlipia kodi? Kwa kweli iliniuma sana”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.