Irene Paul , Haogopi Kuzeeka kwa Sababu ya Kuzaa.
Mwanadada kutoka bongo movies Irene Paul amefunguka na kusema kuwa bado anategemea kuzaa na kuongeza mtoto wa pili na wala hana wasiwasi wa kusema kuwa atazeeka kwa sababu ya kuzaa kwa sababu anaamini kuwa bado ana nguvu ya kuzaa.
Irene anayasema hayo kutokana na ukweli kwamba wanawake wengi hasa katika tasnia yao wamekuwa na tabia ya kuogopa kuzaa kwa sababu ya kuogopa kupoteza muonekano wao , lakini kwake hilo sio tishio hata kidogo.
sina hofu ya kuendelea kuzaa kwamba labda nitapoteza muonekanao wangu, au nitapoteza ustaa wangu,Ninachojua ni kwamba watoto wanakufanya akili yako kuchangamkaa , na kila mtu kwa sasa anajivunia kuwa na watoto wake ni tofauti na pale zamani watoto walikuwa wanafichwa.