Irene Uwoya: Nimeolewa na Mwanaume Wa Ndoto Zangu, Nakupenda Dogo Janja

Muigizaji wa Bongo movie Irene Uwoya hatimaye amefunguka asubuhi hii na kukiri kuwa ameolewa na mwanamuziki wa Bongo fleva, Dogo Janja.

Tangu ijumaa ndoa hiyo ifungwe kumekuwa na utata wa nani ni mume wa Uwoya huku wengi wakiwa hawataki kuamini kuwa mwanamke mrembo kama Uwoya anaweza kuolewa na kijana mdogo kama Dogo licha tu ya utofauti katika umri pia ni kipato.

download latest music    

Leo hii kama dakika ishirini zilizopita kupitia ukurasa wake wa Instagram, Irene Uwoya amemweka wazi mume wake aliyemuoa siku mbili zilizopita ambapo ameandika maneno yafuatayo:

I married the man of my dreams @dogojanja I am still crying happy tears I love you and I am excited to spend the rest of my life with you”.

Kwenye ujumbe huo wa hadhara Uwoya kamfungukia mumewe Dogo Janja kuwa anashukuru amepata mume wa ndoto zake mwanaume aliyekuwa anamuota kila siku na mpaka sahivi akimfikiria bado anatokwa na machozi ya furaha na pia ana hamu kubwa ya kuona maisha yao pamoja yatakavyokuwa pia watakavyoishi pamoja milele mpaka pale kifo kitakavyo watenganisha.

Uwoya amemweka wazi mumewe baada ya watu kuanza kuzusha kuwa ameolewa na kigogo ambaye ana mke na watoto, lakini mpaka sasa bado hajaweka wazi picha zao hizo za harusi zinazowaonyesha wakiwa kwa pamoja.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.