Jacqueline Wolper Akemea Wasanii Wanaovaa Nusu Uchi

Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper amewajia juu wasanii wenzake wa kike ambao mpaka leo wanaendelea na tabia ya kuvaa nusu uchi kwenye mitandao ya kijamii.

Mapema mwaka huu serikali iliingilia kati suala la wasanii kuvaa nusu uchi kwenye mitandao ya kijamii na hata Raisi John Pombe Magufuli aliliongelea hilo suala na hata kusema kuna baadhi ya watangazaji wana tabia ya kuvaa nusu uchi.

download latest music    

Baada ya kutangaza mapambano dhidi ya wasanii ambao wana tabia ya kuimba nyimbo zisizo na maadili ya Kitanzania lakini pia serikali imetilia mkazo suala la mavazi ya heshima kwa watoto wa kike.

Wolper amewatolea povu wasanii wenzake ambao bado wanaendelea kuvaa nguo fupi ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram aliandika maneno haya:

Haki ya kweli yule kiongozi wa kukomesha vichupi yuko wapi? mbona bado tunaona makalio ya watu Instagram? au ndio sanaa every where I go me I wonder mpaka Jasho la damu linanitoka chaaa…..hakuna aliyenihach nauliza swali”.

Mapema mwezi wa jana Naibu wa Waziri habari na sanaa Bi. Juliana Shonza alitangaza vita dhidi ya wasanii wote watakaonekana wanavaa nusu utupu moja kati ya wasanii ambao walitajwa alikuwa msanii Preety Kind ambaye aliishia kufungua kufanya sanaa kwa miezi Sita na Gigy Money.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.