Jacqueline Wolper Amvulia Kofia Harmonize

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Jacqueline Wolper amemvulia kofia aliyekuwa mpenzi wake msanii wa Bongo fleva kutoka WCB, Harmonize na kukubali bifu lao liishe.

Kwa muda wa wiki nzima sasa Wolper na Harmonize wamekuwa Kwenye vita ya maneno Kwenye mitandao ya kijamii huku kila mmoja akidai mwenzake bado anampenda na bado anamtaka.

download latest music    

Wolper ameamua kupiga kimya ili bifu lao lilikuwa linaendelea liishe tofauti na juzi na siku zilizopita ambapo alikuwa akipewa Dongo lolote na Harmonize alikuwa anajibu.

Siku ya jana Harmonize alihaidi kuendeleza mtanange huo baada ya kudai anataka kuweka listi nyingine ya wanaume waliotembea na Wolper baada ya mara ya mwisho kuweka listi ya wanaume kumi na mbili.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Wolper aliandika ujumbe huu kuashiria hatomjibu Tena Harmonize:

Mungu nifundishe kunyamaza, we ndio unaujua ukweli #Najifunzakuheshimkilangaziiliyonifikishanilipo
#NdiomaanataupambanesiwezkushukaatanishushaMungupekee #jifunzekuheshimkilangaziiliyokufishaulipokamweutoteterekakwajarbulolote
#MunguwanguwaushindiwewenijbuToshaNimekukabidhiwewekilakitu

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.