Jay Dee Awatolea Povu Waliomwambia Ajui Kuvaa Kwenye Harusi ya Ay.

Mwanadada anaefanya vizuri katika muziki tangu miaka ya 90 mpaka kufikia hatua ya kumpachikwa jina la dada mkuu katika muziki Lady Jay Dee, amewatolea povu mashabiki ambao walimchamba na kumwambia kuwa amekosea kuvaa na kwamba hajui fashion  kutokana na kuvaa nguo nyeupe katika harusi ya msanii mwenzie Ay iliyofanyika wikiendi iliyopiat.

Lady Jay Dee ambae mara nyingi alishatamka kuwa hapendi kuendeshwa na hisia za mashabiki hivyo anataka kufanya kile ambacho yeye anajiskia anasema kuwa watu wamekuwa wakisema bila kuvaa uhusika wa kile kilichokuwa kinatokea au kufanyika, akijaribu kuweka mfanano wa wageni waalikwa wengine Lady Jay Dee anasema kuwa sio peke yake aliekuwa amevaa nguo nyeupe hivyo watu waache kuongea bila kuwa na uthibitisho.

download latest music    

katika ukuraa wake wa instagram , lady jay dee alitoa povu hili:haya wale mazwzawa wote ambao mlinichamba kuwa kuhusu kuvaa nguo nyeupe kwenye harusi ya watu..oooh kagooglee haya huyo google ni nani? ndo baba yenu au?haya na hao warembo wote waliovaa nyeupe vipi?mambo msioyajua  muwe mnayauliza kwanza kabla kuanza kubwata bwata..tusivae rangi ya harusi kisa nini..kisa google,,hebu mie..

Wasanii wengine wamekuwa wakikerwa na maneno ya mashabiki katika mitandao kwa kile wanachodai kuwa wamekuwa wakiongea na kuwataka  wasanii kufanya vile wanavyotaka wao wafanye.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.