JB Afunguka Baada Ya Kukataa Movie Za Wanigeria “Sitafuti Umaarufu Natafuta Pesa”

Muigizaji mkongwe wa Bongo movie Jacob Stephen maarufu kama JB amefunguka na kudai amekataa kufanya kazi mbili kubwa za Wanaigeria kwa sababu ya pesa ndogo waliyotaka kumlipa.

JB amefunguka hayo Kwenye mahojiano na Bongo 5 ambapo amedai sahivi hatafuti umaarufu wa kuonekana kwenye filamu na Wanigeria bali yupo bize kusaka pesa za ukweli.

download latest music    

Mimi kusema kweli napenda pesa na hata hao Wanaigeria wamekuwa kama mara tatu lakini tuliposhindwana ni kipato tu yaani siwezi kuinuka hapa nikaenda Nigeria halafu nikiangalia pesa ninayolipwa ni  haiwezi kunitosheleza mimi sahivi sahivi sitafuti umaarufu tena natafuta pesa.

Lakini pia  hata ukiniuliza sababu kubwa ya kuacha uigizaji na kuwa producer ni hela tu na siyo kwamba sitamani kuendelea kuigiza ila napata mashabiki zaidi nikiwa producer kuliko muigizaji”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.