Johari Aipa Baraka Zote Ndoa Ya Ray na Chuchu Hansy

Muigizaji wa Bongo movie Johari Chagula ametoa baraka zake zote kwenye ndoa ya Ex wake Ray Vincent Kigosi na mama mtoto wake Chuchu Hansy.

Johari na Ray walikuwa kwenye Mahusiano ya kimapenzi kwa miaka mingi kipindi cha nyuma lakini ameibuka na kuweka wazi kwa hivi sasa hana kinyongo na wapendanao hao kuwa pamoja.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Johari amedai kuwa hakuna kitu kitakachomfurahisha kama mwigizaji mwenzake, Vincent Kigosi ‘Ray’ akimuoa mzazi mwenziye, Chuchu Hansy.

Ray na  chuchu Hansy

Lakini pia Johari ameweka wazi  kuwa Chuchu ni chaguo sahihi la Ray maana ni mwanamke ambaye amemzalia mtoto mzuri.

Kiukweli nitafurahi sana mkurugenzi mwenzangu (RJ Company) akimuoa Chuchu. Kwanza ni mwanamke wa chaguo lake na pia amemzalia kidume cha nguvu na kwenye harusi nitakuwa mstari wa mbele“.

Ray na  Chuchu Hansy wamejaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume anayeitwa Jaden.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.