Johari Akimbia Mjini, Aamua Kufanya Kazi Mikoani.
Mwanadada Blandina Chagula maarufu kama Johari amefunguka na kusema kuwa kwa sasa aanaanza kufanya kazi zake mikoani na sio dar tena kwa sababu kuna vipaji vingi mikoani hivyo ameamua kuznguka huko ili kuvitafuta na kufanya kazi.
Johari anasemakuwa kwa muda mrefu amekuwa Dar wakati kazi za sanaa sasa hivi zinalipa sana mikoani kwa sababu kuna vitu vingi vipya vinatakiwa kuonyeshwa ka mashabiki wao na ndio maana yeye ameamua kufanya kazi huko kuliko kukaa tu mjini.
Ni kweli muda mwingi sasa hivi nazunguka mikoani kwa ajili ya kufanya kazi huko,unajua kwa sasa hivi mikoani sanaa ndio inakuwa kwa kasi kwaio kwa mtu anaejielewa anaweza kutumia fursa hiyo katika kutafuta masoko huko ili kupata fedha kuliko kungangania Dar tu.