Jokate Akimbia Mitandao Ya Kijamii Baada Ya Ali Kiba Kuoa

Msanii na mfanyabiashara maarufu mitandaoni Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ amepotea kabisa Kwenye mitandao ya kijamii tangu aliyekuwa mpenzi wake staa wa Bongo fleva Ali Kiba alivyofunga ndoa.

Jokate na Ali Kiba walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa muda mrefu lakini mwaka jana mwishoni habari zilisambaa kuwa wameachana ingawa hakuna aliyethibitisha taarifa hizo.

download latest music    

Ali Kiba alifunga ndoa na Amina Khalef tarehe April  19 / 2018 Mombasa nchini Kenya na kiukweli Jokate aliandamwa sana na mashabiki juu ya ali Kiba kuoa mwanamke mwingine.

Siku ya shughuli ya Alikiba Jokate aliposti picha katika ukurasa wake wa Instagram na kuambatanisha na caption iliyosomeka; LoL (Laugh Out Loud). Post hiyo ya Jokate ilienda mbali sana baada ya watu kuhusisha na hatua aliyochukua Alikiba ya kufunga ndoa.

Sasa basi, tangu April 20, 2018 siku moja baada ya Alikiba kufunga ndoa Jokate hajaonekana katika mtandao huo wa Instagram, hivyo hivyo katika mtandao wa Twitter na Facebook, mashabiki wanahoji ukimya wake umesababishwa na nini?.

Ingawa na Jokate aliweka wazi siku yake ya birthday kuwa anategemea Kuolewa mwaka huu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.