Joyce Kiria Azidi Kufunguka Mazito Kuhusu Ndoa Yake

Mtangazaji maarufu wa kipindi cha Wanawake Live kinachorushwa na Kituo cha East Africa Tv, Joyce Kiria amezidi kufunguka Mazito Kuhusu ndoa yake na Mwanasiasa wa Chadema Henry Kilewo.

Joyce aliweka wazi hali ya ndoa yake Miezi michache iliyopita ambaoo amedai kuwa Mumewe alikuwa anamnyanyasa na kumtesa na hata kumpa kichapo wakati wa ndoa yao.

download latest music    

Lakini Joyce amedai kuwa tangu ameanika maovu hayo ya mume wake amekuwa akipokea matusi na lugha za kebehi kutoka kwa watu mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii.

Joyce amesema kuwa matusi hayo na lugha za kebehi kwake anaona ni jambo la kawaida na ni afadhali kwake lakini sio kuvumilia maumivu aliyokuwa akiyapata kwenye ndoa yake na mumewe Henry Kilewo.

Nachotaka kusema ni kwamba kwa vile nilichangua hii kazi  ya kuwa sauti za wanawake najua gharama zipo, na gharama kubwa kabisa ni kutukanwa lakini sio kwamba mimi sioni hayo matusi nayaona lakini navumilia. Kwahiyo sio kwamba siumii naumia!! na kuna wengine wananikosesha dili za matangazo kwenye kipindi changu kwa kuona nimejiharibia na mambo ya kisiasa.

Pamoja na machungu yote ninayoyapitia ya kutukanwa na kukosa wadhamini kwenye kipindi changu nikilinganisha na maumivu ya kwenye ndoa ni bora nitukanwe na jamii  lakini sio kuvumilia ukatili na machungu ya ndoa yangu“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.