JPM Ahusika Kufanikisha Safari ya Matibabu ya Majuto Nchini India.
Msanii wa filamu za maigizo na vichekeshao Mzee Majuto amefanikiwa safari yake ya matibabu kwenda nchini india kwa ajili ya matibabu kwa matatizo aliyoyapata alipokuwa nchini kushindwa kufanikiwa hivyo kwenda nchini india .
Akiongea na waandishi wa habari siku ya tarehe 1 May, Steve Nyerere ambae alisaida sana katika zoezi hilo anasema kuwa siku hiyo Mzee Majuto atatarajiwa kusafiri kwenda india kwa ajili ya matibabu yake huku akiwataja na kuwashukuru sana baadhi ya watu waliokuwepo katika kfanikisha hilo huku akiwataja Mh Magufuli na Mh Mwakyembe katika kufanikisha hilo.
niseme ahsante sana kwa mh raiis john pombe magufuli , mh mwakyembe pamoja na Ummy Mwalimu kwa kufanikisha hili, lakini pia niwashukuru wasanii kwa kujitoa kwao, Mungu akipenda leo mzee majuto atakuwa njiani kwenda India kwa matibabu.
Hata hivyo Steve Nyerere pia amewatolea povu baadhji ya wasanii wanaokaa kujinadi katika mitandao kuhusu maisha yao lakini mwisho wa siku wanabaki wakiangaika na kuwa wanaomba misaada wanapopata shida.
Sidhani kama miaka nenda rudi tutakuwa na kazi ya kuwa tunaomba omba tu,tumekuwa watu wa kufanya maparty kila kukicha na kujinadi kuwa ngu zetu za miliona 3, 4 lakini ukimuuliza umejipangaje kwa kesho hamna kitu.