Juma Jux Atinga Ndani Ya Coke Studio

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Juma Jux amefanikiwa kufika katika bonge la shoo la Coke Studio ambalo limeshawahi kuwashirikisha wasanii wakubwa Afrika.

Jux anafanya vizuri na ngoma zake kama vile Zaidii” na “Tell Me”, Lakini mbali ya  muziki, Jux pia ni mfanyabiashara akiwa ni mmiliki wa chapa ya T-shirts “AFRICAN BOY”, ni bidhaa za nguo zinazopatikana Afrika Mashariki zikimilikiwa na mwimbaji pamoja na mtunzi Juma Jux.

download latest music    

Jux amesema kuwa moja ya mipango yake kwa mwaka 2019 ni kufanya nyimbo nyingi za kushirikiana na wasanii kutoka nje ya Tanzania. Katika Coke Studio Jux anashirikiana na mwana dada Shellsy Baronet kutoka Mozambique.

Kwenye interview yake aliyofanya Jux amefunguka Mengi juu ya mara yake ya kwanza Kushiriki kwenye msimu mpya wa Coke Studio:

Coke Studio ni jukwaa zuri kwa wasanii kwani inapelekea kubadilishana tamaduni na nchi zingine; ni kitu  kizuri ambacho nafurahi kuwa sehemu ya Coke Studio.”

JUMA JUX ataiwakilisha vyema chapa ya “AFRICAN BOY” katika jumba la Coke Studio kwa mwaka 2019, kuanzia Februari.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.