Juma Jux: Natamani Sana Kupata Mtoto

Mwanamuziki wa Bongo fleva Juma Jux amefunguka kuhusiana na matamanio yake ya kupata mtoto hivi karibuni.

Jux ambaye anatamba na nyimbo yake ya ‘Fimbo’ inayofanya vizuri kwenye radio station charts na Kwenye mitandao ya kijamii kama Youtube ambako inaendelea kutazamwa zaidi.

download latest music    

Jux anafanya media tour kwa ajili ya kuitangaza nyimbo yake hiyo na kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha redi cha E Fm Kupitia kipindi cha Uhondo, Jux amesema anaona amefikia umri wa kuwa na mtoto.

Jux ambaye yupo Kwenye Mahusiano ya kimapenzi na msanii mwenzake Vanessa Mdee, amefunguka na kusema hivi sasa ana umri wa miaka 28 lakini anatarajia kuiwa akisha fikisha umri wa miaka 30 atakuwa tayari na mtoto.

Yeah sina mtoto lakini Mwenyenzi Mungu akipenda siwezi nikasema siku gani lakini soon tu, Mwenyenzi Mungu akinijalia ninavyotaka mimi itakuwa (na mtoto) lakini ni kitu natamani sana kuwa nacho.

Sio kuzaa tu mtoto, je unazaa na nani na huyu mtu unazaa naye yeye mwenyewe yupo vipi, siwezi nikawa na mtoto na msichana yeyote kwanza, japo sometime huwa inatokea ila nakuwa makini sana sana”.

Siku za nyuma habari zilishawahi kuvuma kuwa Vanessa ni mjamzito habari ambazo mwenyewe aizikataa na kusema hana mpango wa kuzaa sasa hivi kwani ana malengo mengi na mziki hajayafikia bado.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.