Jumba La Mobetto Alilozawadiwa na Diamond Lagubikwa na Utata

Wiki iliyopita habari zilienea Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Diamond amemnunulia mjengo wa fahari mama mtoto wake na Hamisa Mobetto ambapo Mama Mobetto alithibitisha taarifa hizo.

Lakini hivi sasa Global Publishers wanaripoti kuwa Habari hiyo siyo ya kweli kwani kwa taarifa waliyokuwa nazo ni kuwa nyumba ile haijanunuliwa bali imepangishwa tu kwa muda.

download latest music    
Baada ya Tetesi hizo gazeti hilo lilienda kufanya uchunguzi ambapo Jirani mmoja wa Mobeto aliyeomba hifadhi ya jina, alipoibukiwa na wanahabari wetu, aliweka wazi kuwa nyumba hiyo hajanunuliwa na ameshangazwa na habari kwamba amenunuliwa.

Kwa kweli nimeamini hawa mastaa wanapenda kujikweza, yaani nyumba hii tumeona mchakato wote na mwenye nyumba tunamjua lakini mitandaoni tunaona mama Mobeto anasema Diamond kawanunulia”.

Lakini baada ya taarifa hizo gazeti hilo lilimsaka mmiliki wa mjengo huo ili aweze kuthibitisha taarifa hizo ndipo ndugu wa mmiliki alipofunguka:

Mimi mwenyewe niliona kwenye mtandao kwamba wamenunua, nikashtuka sana ikabidi niende kumuonesha babu (mmiliki), akasema si kweli ndipo wakapuuza tu maana“.

Mama mzazi wa Mobetto anayejulikana kama Shufaa Rutiginga aliweka wazi Kwenye mahojiano na Wasafi Tv kuwa Diamond alinunua mjengo huo maalumu kwa ajili ya mtoto wake Dyalan.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.