Jux Kuja na Kazi Mpya Baada Ya Kumalizana na Vanessa

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Juma Mussa maarufu kwa Jina lake usanii kama Jux amefunguka kuhusu kuweka kando Tour yake na kuendelea na projects zake.

Baada ya kufanya vyema Kwenye ziara yake ya ‘In Love and Money’ aliyofanya pamoja na mpenzi wake na staa wa Bongo fleva Vanessa Mdee Jux ametangaza kufanya kazi zake mwenyewe.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Jux amesema kwa sasa anadili zaidi na kuten­geneza nyimbo zake yeye kama yeye na kuweka pembeni kwa muda suala la tour yao hiyo.

Kwa sasa ninataka kuja na pro­jekti zangu mimi kama mimi na siyo tena na Vanessa kama ambavyo tume­kuwa tukifanya kwenye hii tour ya In Love With Money, nina­chofanya ni kutengeneza video na nyimbo zangu.

Unajua hiyo tour haijafika mwisho, tutaendelea kuifanya ila kwa sasa ninafanya mambo yangu kama mimi kisha baadaye tena tu­tarudia kuzunguka mikoa mbalimbali”.

Jux na Vanessa walitangaza kuongeza mikoa ya kufanya ziara yao baada ya mikoa ya Mwanzoni kufanya vyema sana na kuuza ticketi zote.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.