Jux na Vanessa Watangaza Shoo Nje Ya Nchi Baada Ya Mafanikio Makubwa Nchini

Mastaa wa muziki wa Bongo fleva ambao pia ni wapenzi Juma Jux na Vanessa Mdee ‘Vee Money’ wametangaza kuipeleka tour yao nje ya nchi baada ya kupata mafanikio makubwa nchini.

Wasanii hao wamekuwa wakifanya tour yao ya ‘In Love and Money’ katika mikoa mbali mbali ya Tanzania kama vile Mwanza, Dodoma na Arusha na baada ya kupata mafanikio makubwa katika mikoa hiyo michache wametangaza Tour hiyo nchi za nje.

download latest music    

Nchi ambazo Jux na Vanessa wataenda kupiga Tour hiyo ni pamoja na Rwanda, Burundi na Congo mara tu baada ya kumaliza show yao ya mwisho Jijini Dar es salaam.

Jux amefunguka na kuiambia Wasafi Tv, mara tu baada ya Kumaliza shoo yao iliyofanyika mkoani Arusha:

Hii show inaendelea tukitoka Dar tunaenda Rwanda, tukitoka Rwanda tunakwenda Burundi na tukitoka Burundi tunakwenda Congo.”

Jux na Vanessa wamekuwa wakipata mapokezi makubwa sana kutoka kwa mashabiki zao katika mikoa yote waliyofanya shoo hizo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.