Kajala Na Zari Wasemekana Kuwa Na Siri Nzito

Ikiwa ni kama wiki imeshapita tangu kufanyika kwa harusi ya  Rommy Jons ambae ni Dj  wa msanii maarufu na mkubwa Tanzania Diamond Platinumz  ambae pia ni ndugu yake ambae wamekuwa wakifanya kazi pamoja , siri imevuja kuwa katika watu waliohudhuria akiwemo Kajala na mzazi mwenzie na Diamond anaejulikana kama Zari The Bossy wamekuwa wakikwepana na hilo lilionekana live siku ya harusi.

Wanawake hao ambao kila mmoja amekuwa nguli katika mitandao kwa nafasi yake na warembo wamesemekana kukwepana hasa Kajala ambae aliamua hadi kutoka kabisa katika sherehe hiyo  baada ya kuona kuwa kitendo cha yeye kwenda mbele kingemkutanisha kwa karibu na Zari The Bossy.

download latest music    

Katika harusi hiyo kuna wakati ambapo Mc aliwahitaji baadhi ya watu mbele kwa ajili ya ufunguzi wa champaign  mabapo kati ya watu hao walitajwa ni pamoja na Zari na baadae alimuita kajala ili aweze kujumuika pale mbele kwa ajili ya kufungua shampeni lakini kitu cha ajabu na ambacho si cha kutegemea Kajala aliamka na kupitia mlango wa nyuma na kutokomea kusiko julikana ilhali sherehe ikiwa bado haijaisha na kuwaacha watu wakisubiri kutokea kwake.

Hata hivyo baada ya kajal kutafutwa ili kuweza kuthibitisha hilo alikubali kuwa ni kweli aliamua kuondoka kwa sababu alikuwa hataki kuonana na baadhi ya watu, swali linakuja kwanini alikwenda kwenye harusi ilihali alijua hataki kuonana na baadhi ya watu na akiuja kabisa ni harusi ilipaswa kuhudhuriwa na watu maarufu, lakini pia kwanini iwe katika kipindi cha ufunguzi wa shampeni tena baada ya kuitwa mbele yeye na Zari.

ni kweli nilikwenda kwenye hiyo harusi  na nikaitwa mbele lakini niliamua tu kuondoka zangu kwa sabau sikutaka  kuonana na baadhi ya watu  .-Alifunguka Kajala.

Wawili hao hawajawahi kusikika kuwa wamegombana hata siku moja hivyo kama ni maadui basi kuna kinachoendelea kati yao ambacho hakijawahi kuweka wazi na watu hao wawili  na kuamua kufanya siri kwa maslahi yao binafsi.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.