Kajala- Sina Urafiki na Wema, Nina Marafiki Wapya

Muigizaji wa Bongo movie Kajala Masanja amefunguka kuhusu urafiki wake na msanii mwenzake Wema Sepetu na kudai kwa sasa hawana urafiki tena.

Wema na Kajala walikuwa marafiki wakubwa sana mara baada ya Wema kumlipia Kajala shilingi milioni 13 katika kesi yake lakini urafiki huo ulivunjika baada ya Kajala kumsaliti Wema na kumuibia mwanaume wake.

download latest music    

Baada ya uadui wa miaka kadhaa mwaka jana Wema na Kajala walionekana kulimaliza bifu lao baada ya Wema kumtumia Kajala salamu za siku ya kuzaliwa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers  Kajala anaweka wazi kuwa hana urafiki na Wema na kusisitiza ana rafiki yake mwingine ambaye amemtaja:

Kuhusu suala la urafiki wangu na Wema yameshapita hayo na mimi kwa hivi sasa nina marafiki zangu wengine kabisa na rafiki yangu kipenzi ambaye anajua mambo yangu yote ni Lamata”.

Lakini pia Kajala alikataa Tetesi za kutaka Kuolewa na Kigogo hivi karibuni lakini amekiri ana mpango wa unalipa Kwenye mjumba wake wa kifahari.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.