Kala Jeremiah Akana Kuwa na Bifu na Roma

Msanii mkongwe wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kuchana Kala Jeremiah amekana kabisa tetesi zinazodai kuwa ana bifu na Msanii mwenzake Roma Mkatoliki.

Habari za wasanii hao kuwa na bifu zilianza baada ya wasanii hao kupunguza ukaribu waliokuwa nao zamani na hata kutopeana sapoti katika kazi zao Ikiwa ni pamoja na kutopostiana Kwenye mitandao ya kijamii.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Roma amedai kuwa hana bifu lolote na Roma bali ni marafiki wazuri bado:

Hapana sina bifu na R.O.M.A yeye kwangu ni kama ndugu na hatuna tofauti zozote zile na sina background hasa ishu hiyo iliibukia wapi.

Hatuna bifu. Kwanza R.O.M.A kwa sasa ana kundi, kwa hiyo muda mwingi unakuta anafanya mambo yake na kundi lake. Hatuambatani tena ni kama ambavyo unaweza usimuone R.O.M.A na ndugu yake yeyote wakimbatana, lakini ukamuona na Stamina. Utasema haelewani na ndugu zake? Kuna muda tunaonana na mambo mengine yanaendelea, lakini si kwamba tuna tofauti. Kuhusu mitandaoni, ukitazama Instagram, kwanza ni kama hayupo vile, kwa hiyo tupo sawa”.

Lakini pia Kala alicheka baada ya kusikia tetesi kuwa eti hawaelewani sababu ya penzi la Dayna Nyange ambapo amesisitiza kuwa wapo vizuri tu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.