Kassim Mganga Awataka Mastaa Wote Wanaoishi Na Wapenzi Mwezi Huu Waache

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Kassim Mganga amewatolea povu wasanii au mastaa wote ambao wanaishi na wapenzi wao mwezi huu waache.

Ukiwa ni mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo waislamu wote duniani wanafunga kwa kuomba dua kwa Mwenyezi Mungu, wanahimizwa kufanya matendo mema.

download latest music    

Kassimu Mganga amewataka mastaa wenzake wauheshimu mwezi hasa kwa wale ambao bado mpaka sasa hivi wanaendelea kuishi na wanawake/ wanaume ambao sio wake/ waume zao Kwenye mwezi huu.

Kwenye mahojiano na Sam Misago Tv, Kassimu alifunguka haya:

Sio mimi ninayesema haya lakini ni agizo la Mwenyezi Mungu kwaiyo inapokuwa halitekelezwi inakuwa haipo sawa kwani kuna umuhimu mkubwa wa kuweza kuheshimu maandiko hasa huu mwezi ingawa najua wengi wetu bado vijana na wengi bado hawajaoa kutokana na kwamba hawajajipanga na wengine wakati bado lakini unaweza ukaupisha Kwanza mwezi ukapita baada ya hapo ukaendelea”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.