Kesi ya Babu Tale Yaonekana Kuwa Bado Ngumu.
Kesi inayomkabili meneja ya tip top connection babu tale bado inaonekana kuwa ngumu kutokana na uzito wake baada ya wawili hao kuitwa tena mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo.babu tale ambae anashitakiwa na mahakama akisimama kamammwakilishi wa tip top connection kwa kosa la kurudufu cd za mawaidha ya shekhe huyo bila ridhaa yake .
Hata hivyo hukumu ya kesi hiyo iliyowahi kutolewa hapo kabla ilimtaka babu tale kutoa fidia ya milion 250 kwa shekhe huyo lakini babu tale hakutekeleza swala hilo.
Kesi inazidi kuwa nzito kwa sababu hakimu aliyetoa hukumu hiyo inasemekana alisaidi hati ya hukumu hiyo akiwa amekwisha staafu na kwamba hata msajili wa mahakama aliyesimamia kesi hiyo hana mamlaka ya kutoa hukumu ya kufungwa kwa mshtakiwa .
Hata hivyo baada ya mvutano wa muda mrefu, mahakama imepanga kukutana tena na pande zote mbili juni 25 mwaka huu tena.