Kesi ya Lulu Yaendelea Kuunguruma ( Tazama Video ya Lulu Akitimua Mbio Mahakamani)

Kesi ya mauaji bila kukusudia inayomkabili muigizaji Lulu Michael imehairishwa mpaka tarehe 25 Oct siku ya kesho ambapo shahidi ambaye ni mke wa Dr. Slaa, Dr. Josephine Mshumbusi kutofika mahakamani kutoa ushahidi.

Josephine Mshumbusi alikuwa mmoja wa madaktari waliomtibu marehemu Kanumba, ameshindwa kufika mahakamani siku hii ya leo kutokana na kwamba yuko nje ya nchi na hivyo kusababisha mawasiliano kuwa magumu, hivyo mahakama ikawa imeomba maelezo ya bi. Josephine  yaliyoandikwa polisi siku ya tukio hivyo siku ya kesho inategemewa askari aliyeandika maelezo hayo kufika mahakamani na kutoa ushahidi huo.

download latest music    

Hapo Jana wakili wa mshtakiwa, Peter Kibatala aliomba mahakama ikubali kupokelewa kwa ushahidi utakaotumwa na bi. mshumbusi ambaye yupo nje ya nchi kwa sasa lakini mahakama ilikataa ombi hilo na ikasema upande wa utetezi hauwezi kusoma ushadi huo na kuagiza askari aliyeandika ushahidi huo awepo mwenyewe.

Baada ya kesi hiyo kuairishwa leo asubuhi Lulu amejikuta katika wakati mgumu baada ya kutimua mbio huku waandishi wa habari wakimkimbiza ili kupata picha hizo tafadhali tazama video hiyo hapa.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.