Kifesi Adai Diamond Amepoteza Kitu Cha Thamani Maishani Kwa Kumpoteza Zari

Aliyekuwa mpiga picha wa staa wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz, Kifesi amevunja ukimya na kufunguka kuhusu kuvunjika kwa Penzi la Diamond na Zari.

Kifesi aliacha kazi WCB Miezi michache iliyopita lakini ilisemekana kuwa amefukuzwa kazi na Diamond baada ya kuingilia kati Penzi la Diamond na Zari.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Kifesi amefunguka na kuweka wazi kuwa Diamond amefanya makosa kuachana na Zari kwa sababu ni mwanamke anayejielewa sana.

Mimi naamini Diamond amefanya makosa sana kuachana na Zari kwa sababu Mwanaume yoyote mwenye akili na Basara atamuona Zari kama aina ya mwanamke ambaye anatamani awe naye kujenga maisha na kujenga familia.

Kwaiyo Diamond atakuwa ni wa ajabu kama akisema eti hajapoteza kitu cha thamani kwa kumpoteza Zari nitamshangaa halafu hata yeye anaelewa umuhimu wake ukilinganisha na wanawake ambao ameshawahi kuwa nao na hata alionao huwezi ukawalinganisha na Zari”.

Kifesi pia amekiri kuwa hana mawasiliano yoyote na Diamond tangu aache kazi WCB Miezi michache iliyopita lakini bado ana ukaribu na urafiki na Zari na anaongea naye kila siku.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.