Kifesi Afukuzwa Kazi na Diamond Baada Ya Kumshauri Arudiane na Zari

Mpiga picha maarufu wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Kifesi amedaiwa kufukuzwa kazi WCB baada ya kumshauri bosi wake arudiane na Zari.

Kifesi alitumia ukurasa wake wa Instagram na kutangaza kuwa ameamua kuacha kazi kama mpiga picha wa Diamond na kujiajiri mwenyewe na kudai anataka kuwa karibu zaidi na Mungu wake kwa kupitia dini yake.

download latest music    

Lakini Mara tu ya habari hiyo kusambaa taarifa mbali mbali kutoka kwa watu wa karibu wa WCB walianza kudai kuwa Kifesi hajaacha kazi bali ametimuliwa na Diamond kwa tabia yake ya kupenda kuingilia maisha binafsi ya bosi wake Diamond.

Kifesi ni mtu ambaye huweka wazi siku zote kuwa anampenda Zari name hata siku alipomuacha Diamond alidai hata Kama wameachana lakini yeye bado anampenda Mama T na kumkubali.

Sasa juzi juzi baada ya Zari kuja Tanzania kusaini dili lake jipya Kifesi alitumia nafasi hiyo kumshauri tena Diamond arudiane na Zari kitendo kinachisemekana kuwa hakikukaa vizuri na Diamond ambapo aliishia kumfukuza kazi.



About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.