Kifesi-Tangu Nimeacha Kazi WCB Diamond Hajawahi Kunitafuta

Aliyekuwa mpiga picha wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Kifesi amefunguka na kudai tangu ameacha kazi WCB, Diamond hajawahi kutafuta zaidi alim-block Instagram.

Miezi michache iliyopita Kifesi alitangaza kuwa anaacha kazi WCB baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu ambapo alidai sababu kubwa ilikuwa ni kutaka kufungua biashara zake na kujikita Kwenye mambo yake kidini.

download latest music    

Baadae kuna taarifa zilisambaa kuwa Kifesi hajaacha kazi WCB bali alifukuzwa kazi na Diamond  kwa utovu wa nidhamu baada ya kudaiwa kuingilia mapenzi ya bosi wake (Diamond na Zari).

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Kifesi amefunguka na kuweka wazi kuwa tangu ameacha kazi WCB, Hajawahi kuwasiliana na Diamond na pia kukiri kuwa Diamond amemblock Instagram.

Lakini pia Kifesi amesema yeye binafsi hana beef na Diamond na hawezi kuongelea mabaya yake kwa sababu tu hayupo naye karibu na kudai yeye ni mtu mwaminifu na anampenda Diamond kama shabiki.

Kwenye Interview hiyo Kifesi aliongelea Tetesi za yeye kufukuzwa kazi ambapo amedai kama kweli angekuwa amefukuzwa basi watu wangemuona amempigia magoti Diamond amrudishe kazini na kama haitoshi angemtumia Zari ambaye amekiri Diamond hapindui kwa Zari.

Kifesi ameongelea biashara zake mpya ambapo amefungua studio ya upigaji picha na yupo mbioni kuanza kipindi chake cha mapenzi redioni lakini pia anafungua kampuni yake ya kuuza chakula.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.