Kifungo Cha Lulu Watu Wamegeuza Ushabiki na Biashara- Belle 9

Msanii wa Bongo fleva anayejulikana kama Belle 9 amefunguka kuwa amesikitishwa na kifungo cha Lulu lakini yeye ameamua kukaa kimya juu ya suala ilo kwa sababu ameona watu wengi wamegeuza ushabiki.

Tangu kifungo cha miaka miwili cha muigizaji Lulu Michael kitangazwe siku ya Jumatatu mastaa mbalimbali wamekuwa na maoni tofauti na hata wengine kubishana baada ya kugawanyika huku wengine wakiwa upande wa Lulu huku wengine wakiegemea upande wa Kanumba. Wasanii kama Mrisho Mpoto na Afande Sele wameingia katika majibizano makali mtandaoni baada ya kila mmoja kuegemea upande wake na kuamini anachotaka kuamini.

download latest music    

Belle 9 alipohojiwa na Millard Ayo Tv aliweka wazi hisia zake na kusema kuwa kwake yeye imekuwa ngumu kuongea chochote juu ya kesi hiyo siku hizo zilizopita kwani anaamini kuwa kuna wasanii wanashabikia kesi hiyo kwa sababu zao binafsi:

Unajua ishu ya Lulu ni ishu ambayo wakati inatokea watu wengi walionyesha sana ushabiki kwa upande fulani kwaiyo mimi nilivyoona ile hali ya kama kuna mgawanyiko na utimu sikupenda kuongea kitu kwa kweli kwa sababu ningeoneana kama naegemea upande fulani, Lakini kiukweli iliniuma kama msanii mwenzie kama mtu ambaye huwa anasapoti kazi zangu na tupo vizuri wakati wote hata tukikutana ni mtu ambaye tunapiga stori freshi tu lakini nilivyoona tu haya mambo ya ushabiki nikaona niache tu maana kuna watu huko mtaani wakiona umeegemea upande wa Lulu au upande wa Kanumba wanakutenga”.

Pia Belle 9 aliwasihi wasanii wasigeuze kifungo cha Lulu kama njia ya kufanyia bishara au upepo fulani wa trending ili tu waonekane mbele za watu kuwa bado wapo kwenye ramani.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.