Kitabu Cha Mapenzi Cha Shilole ‘Broken Heart’ Chazua Gumzo

Msanii maarufu wa Muziki na mjasiriamali Shilole a.k.a Shishi Baby ametangaza ujio wa Kitabu chake kiitwacho Broken Heart alichoandika na mwandishi chipukizi Jackson Fute.

Shilole akiwa na Mwandishi wa Kitabu, Jackson Fute

Taarifa ya Kitabu hicho alizianika Instagram alipoweka picha za yeye na mwandishi huyo wakiwa na mameneja wao Mc Carter na Viola Julius wakisaini mkataba wa makubaliano.

download latest music    

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Shilole pia aliandika:

Kabla ya kitabu hakijatoka tunaweka mambo sawa. Kisheria zaidi leo nimemalizana na na Jackson Fute kuhusiana na Kitabu Chetu cha Broken Heart”.

Kitabu hicho kimezua maswali mengi sana kwani mpaka hivi sasa hakuna anayejua nani hasa ataandikwa Kwenye Kitabu hicho cha mapenzi kama atakuwa Nuh Mziwanda au Uchebe.

Lakini pia Shilole ameweka wazi kuwa Kitabu hicho kitatoka siku yoyote kuanzia sasa kwani uandishi wa Kitabu umekwisha kamilika.

Usiri wa kilichoandikwa ndani ya Kitabu hicho ndio kinatupa hamu ya kutaka kujua na kukisoma, tusubiri taarifa zaidi ya uzinduzi wa Kitabu hicho.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.