Kocha Julio Ataka Kumsajili Alikiba Katika Timu Zake.
Baada ya kumalizika kwa mechi ya kirafiki kati ya timu ya Alikiba na timu ya Mbwana Samatha ailiyofanyika uwanja wa taifa jumamozi iliyopita. kuekuwa na maoni mengi sana kuhusu mechi hiyo huku wakifurahi na kuwashukuru watu wote waliojitokeza kuangalia mechi hiyo iliyokuwa na lengo la kutumia pesa zilizopatikana kwa ajili ya kusaidia elimu katika shule zenye mazingira magumu.
Katika moja ya maoni yaliyojitokeza ni kuhusu alikia kutoka kwa kocha Jamhuri Kiwhelu maarufu kama Julio aliyekuwa kocha kutoka upande wa Alikiba huku akisema kuwa msanii huyo ana uwezo mkubwa sana wa kucheza mpira laki i amekuwa akimshawishi kufanya mpira na amekuwa akimkatalia kila mara.
mara nyingi nimekuwa nikimwambia alikiba aje nimsajili katika timu ninazofudisha ila hatokuwa akicheza mikoani mpaka timu itakapokuwa ikicheza dar es salaam ndio aje kucheza.ninachoweza kusema ni kwamba alikiba ni mchezaji ambae akipata mwalimu anaejua kufundisha kama mimi anaweza kuwa mchezji mzuri sana .