Kolabo Yangu na Ali Kiba Imenipa Mafanikio Makubwa-Nuh Mziwanda

Mwanamuziki wa muziki wa Bongo fleva Nuh Mziwanda amefunguka na kudai wimbo wake wa ‘Jike shupa’ aliomshirikisha Ali Kiba ndio wimbo wake uliompa mafanikio makubwa.

Mwezi uliopita Nuh Mziwanda alianika Rasmi mjengo wake mpya ambao alikuwa anajenga na sasa anaweka wazi kuwa pesa za mjengo huo zinatoka katika ile Kolabo na Ali Kiba ambayo ilimpa Tour nchi nzima.

download latest music    

Nyumba ni yangu na katika ujenzi nilikuwa namshirikisha sana mama yangu, yeye ndio aliyekuwa anashughulika na mafundi. Mimi sikuwa nafuatilia, kipindi kile ndio nilikuwa nimeachia Jike Shupa, nilifanya tour Tanzania nzima, chaka to chaka wilaya kwa wilaya.

Nilikuwa nikipata pesa yangu kidogo kidogo namtumia mama anajenga, kwa hiyo mimi narudi huku nakuta nyumba imefika sehemu nzuri kwa sababu nakumbuka nilikaa miezi mitatu”.

Kolabo hiyo ndio moja ya nyimbo pekee ya Mziwanda aliyofanya vizuri kwani ina viewers milioni mbili Kwenye mtandao wa Youtube.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.