Kuhusu kutoka na msanii wcb,vannessa aongea

Ule uvumi wa muda mrefu ambao umekuwa ukiendelea sehemu mbalimbali katika mitandao unaomhusu msanii wa kike anaetamba na kibao chake ‘KISELA’ vannesa mdee kuwa kwa sasa anatoka na msanii mwenzie kutoka katika lebel ya wasafi (WCB) utakuwa sasa umeeleweka baada ya msanii huyo kutoa yaliyopo moyoni kuhusu maneno hayo.

Akiongea katika interview na ayo Tv ,Vee money anasema kuwa ‘Ninazushiwa ninatoka na watu kila sehemu mwanangu..ndio maana inaitwa ni uzushi” hivyo basi kwa maneno hayo ambayo ameongea yeye mwenyewe vannesa ni dhahiri kuwa maneno yanayosambaa mitandaoni kuhusu yeye ni uzushi mtupu hakuna ukweli ndani yake.

download latest music    

Hata hivyo itakuwa ni mapema sana kwa msanii huyo kuwa wazi juu ya mahusiano yake mapya kwani ni muda mchahche tu uliopita vee ametoka kuachana na mpenzi wake juma jux,hata hivyo baada ya kuulizwa na mwandishi kuhusu swala la yeye na juma jux vannesa alijibu hivi’sisi saivi tunaelewana sana na tumekuwa na maongezi kuhusu swala hilo” hivyo basi inawezekana wawili hao wapo katika harakati za kurudisha mahusiano yao kama mwanza ilihali vannesa anasema wapo katika maongezi.

Kumekuwa na comments nyingi sana kutoka kwa mashabiki kuhusu wawili hao wakiwashauriwa na kuwaomba wawili hao kurudisha mapenzi yao kama awali maana ni moja kati ya couple iliyokuwa inatrend sana na kuonekana kupendeza wanapokuwa pamoja,ivyo labda basi wasanii hao wanafata nguvu ya mashabiki na kukaa pamoja ili kumaliza tofauti zao.

Alipoulizwa kuhusu kuolewa na kuzaa ,vee money alisema kuwa yeye kuzaa bado sana na  kwa sasa  yupo single

Mahusiano ya vannesa na jux yalikuwa ni moja kati ya couple iliyovutia mashabiki wengi,hata hivyo wawili hao walikuwa wakionekana vizuri pamoja na kufikia hatua ya kutoa mpaka nyimbo pamoja,na hata baada ya mahusiano yao kuvunjika jux aliamua kumuimba wimbo mpenzi wake huyo kuonyesha ni jinsi gani bado anamuhitaji,nasi kama mashabiki tunawatakia maongezi mema na tunaimani watarudisha kile walichokuwa nacho hapo awali.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.